Latest Stories

TOP 5 Most Popular Post

Recently Comments

FFFFFFFFFFFFF

FFFFFFFFFFFFF
XXXXXXXXXXX

FFFFFFFFFFFFF

FFFFFFFFFFFFF
XXXXXXXXXXX

Dr. Asha Rose Migiro aagwa rasmi umoja wa mataifa 0 Comments

By Unknown
Wednesday, June 13, 2012 | Posted in ,

Hatimaye aliyekuwa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa Dr.Asha Rose Migiro ameagwa rasmi baada ya kumaliza mda wake katika umoja wa mataifa.Dr Migiro ametumikia umoja wa mataifa kwa miaka mitano tangu kuteuliwa kwake mwaka 2007.
Akizungumza wakati wa  tafrija hiyo, Katibu Mkuu Ban ki Moom ameleezea baadhi ya  sababu  zilizomsukuma  kumteua Dkt. Asha- Rose Migiro kuwa msaidizi wake wa karibu.
 “ Nilianza kumfahamu Asha- Rose Migiro wakati huo sote tukiwa mawaziri wa mambo ya nje  katika nchi zote. Uwezo wake na uelewa wake wa mambo ulinivutia sana, lakini nilivutiwa zaidi pale nilipofahamu kwamba aliwahi kuwa waziri anayehusika na masuala ya wanawake na watoto. Nikajiridhisha kwamba huyu ndiye alikuwa ananifaa kuwa msaidizi wangu wa karibu” akasema Ban Ki Moon na kuufanya umati ulihohudhiria tafrija hiyo kushangilia kwa nguvu.
 Kama hiyo haitoshi, Ban Ki Moon amemuelezea Dkt. Asha- Rose Migiro kama msaidizi wake wa karibu ambaye licha ya kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa lakini ni mtu ambaye alikuwa hana makuu na wala hata siku moja hakujikweza.
 
“ Katika kipindi chote ambacho Migiro amekuwa msaidi wangu wa karibu, amenisaidia katika mambo mengi, ni mtu muadilifu sana, ni mtu aliyekaribu sana na watu, aliyeamsha matumaini na kuwapa tabasamu watu waliokuwa katika mazingira magumu.  Daima amekuwa mstari  wa mbele kunisaidia  na hakuna hata siku moja alipojikwenza. Na kwa sababu hii  anastahili tafrija hii” akasisitiza Ban Ki Moon.
Aidha Ban Ki Moon akamuelezea  Asha- Rose Migiro kama kiongozi ambaye daima alitoa kipaumbele  cha aina yake katika masuala ya afya ya jamii  eneo alilotumia uwezo wake wote, maarifa yake yote kama naibu katibu mkuu kupigania afya ya wanawake na watoto na watu wote walio katika mazingira magumu
Kwa upande wao waandaaji  wa tafria hiyo na wakizungumza kwa nyakati tofauti wamemuelezea  Naibu Katibu Mkuu, kama kiongozi ambaye mchango  wake umesaidia sana katika  kuihamasisha jumuiya kimataifa kuweka mkazo wa aina yake katika kushughulika afya ya jamii.
Aidha  Migiro amewashukuru kwa moyo wa dhati wasaidizi wake wa karibu  aliofanya nao kazi akiwa naibu katibu mkuu na kwamba bila wao asingefika hapo alipo, akawashukuri pia wadau mbalimbali wakiwamo mabalozi kwa ushirikiano wa hali na mali waliompatiwa muda wote wa miaka mitano na nusu.



Follow any responses to the RSS 2.0. Leave a response

Leave a reply

0 comments for "Dr. Asha Rose Migiro aagwa rasmi umoja wa mataifa"