Dc Makonda atoa siku 14 ujenzi wa barabara Kinondoni kukamilika, wahusika wote kuwajibishwa
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda
alifanya ziara ya kutembelea katika maeneo mbalimbali ya Wilaya yake na
kushuhudia kero za uharibifu wa miundombinu ikiwepo barabara na kuamua
kutoa agizo kwa Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha inafanya ukarabati huo ndani ya siku 14 kabla ya kuwawajibisha.
Makonda amesema ‘Nimejionea
ubovu wa barabara za Kinondoni, lakini hii si’mara ya kwanza, mara ya
kwanza niliona ubovu huu na nikaunda kamati ya wataalam wakachunguza na
kubaini barabara nyingi zilijengwa chini ya kiwango‘
‘Hatua
hii ilipelekea kusimamishwa kwa baadhi ya watumishi, lakini cha ajabu
barabara zinazidi kuwa mbovu na wananchi wanalipa kodi, nimejionea pale
Hospitali ya Mwananyamala mama mmoja akijifungulia kwenye bajaji, mbaya
zaidi juzi kuna ajali imetokea na mtu akafa‘
Nini maamuzi yake baada ya haya yote? ‘Sasa
nimeiagiza Manispaa, nimewapa wiki mbili kuhakikisha mashimo yote yawe
yamezibwa, na wakishindwa nitawasaidia kuwawajibisha na kuchukua hatua
stahiki‘ Paul Makonda
Ilikupita hii Video ya Dc Makonda akitangaza Walimu Dar kupanda daladala bure…?
0 comments for " "