Latest Stories

TOP 5 Most Popular Post

Recently Comments

FFFFFFFFFFFFF

FFFFFFFFFFFFF
XXXXXXXXXXX

FFFFFFFFFFFFF

FFFFFFFFFFFFF
XXXXXXXXXXX

0 Comments

By Mpwapwa kona
Thursday, April 21, 2016 | Posted in ,

BWAWA LA KUZALISHIA UMEME KIDATU LAZIDIWA NA MAJI

Bwawa la kuzalisha umeme kwa maji la Kidatu mkoani Morogoro limezidiwa na maji na kulazimu Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kushirikiana na Serikali kufungulia maji yaliyozidi na kuanza kupita katika geti kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.Hatua hiyo imetokana na iwapo wataacha yaendelee kutoka bila kuyadhibiti taratibu itasababisha uharibifu wa miundombinu na kuhatarisha maisha ya watu. Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba alisema maji ya bwawa hilo yamekuwa mengi hivyo yanaweza kuathiri usalama wa bwawa, kwani limetengenezwa kupokea kiasi fulani cha maji hivyo yakizidi presha yanagonga kwenye kingo na yanaweza kusababisha maafa.Mramba alisema pia maji yanapotoka katika bwawa hilo na kurudi mtoni yanaweza kusababisha madhara kwa wananchi wanaofanya shughuli mbalimbali kwenye mto, hivyo ni vema kuyadhibiti.Alisema bwawa hilo limefurika maji licha ya kuzuia maji ya bwawa la Mtera yanayoingia humo kufungwa kwa zaidi ya wiki mbili na mashine zote nne za kuzalisha umeme kuendelea kuzalisha umeme kwa kiwango cha juu.

Follow any responses to the RSS 2.0. Leave a response

Leave a reply